Subscribe:

Ads 468x60px

Wednesday 23 May 2012

DIDA AWAUZIA WAKE ZA WATU NYETI BANDIA

MTANGAZAJI wa Radio Times FM ambaye pia ni mjasiriamali, Hadija Shaibu ‘Dida’ anatajwa kuwauzia wake za watu nyeti bandia za kiume ambazo huzitumia kukata kiu zao.
Chanzo chetu ambacho ni mmoja wa wateja wa Dida kilichojitambulisha kwa jina la Mama Asuu wa Magomeni kimeliambia Ijumaa juzikati kuwa, yeye aliwahi kununua kifaa hicho kwenye duka la Dida lililopo Kinondoni jijini Dar.
“Mbona wanawake wengi wanajazana pale kununua kifaa hicho, niliwahi kumuuliza kama anavyo akaniambia nimpe fedha akienda China ataniletea, juzi ndiyo nikaenda kukichukua,” alisema mama huyo.
Katika kujua ukweli wa habari hizi mwandishi wetu alimtafuta Dida na alipopatikana alisema: “Huwa nikisafiri kwenda kuchukua mzigo China kuna wanawake huniagiza vifaa hivyo lakini kama ni suala la wanawake kujaa dukani kwangu wanafuata vingi.”

1 comment: